Kurasa

Jumamosi, 10 Septemba 2016

Moto wa kiwanda wawaua watu 20 Bangladesh

Moto huo ulisambaa kwa haraka katika nyumba hiyo ya ghorofa nneMoto huo ulisambaa kwa haraka katika nyumba hiyo ya ghorofa nne 
Watu ishirini wameuwawa nchini Bangladesh katika moto mkubwa katika kiwanda kimoja, uliosababishwa na mlipuko wa kifaa cha kuchemsha maji.
Zaidi ya watu 70 wamejeruhiwa viungani mwa mji mkuu Dhaka, na inaarifiwa kwamba huenda idadi ya walioaga ikaongezeka.
Polisi wanasema kwamba zaidi ya watu 100 walikuwa wakifanya kazi katika kiwanda hicho, na kwamba moto huo ulisambaa kwa kasi katika jengo hilo la ghorofa nne.

 Wazima moto wakiwabeba waathiriwa kwenye ajali hiyo ya motoWazima moto wakiwabeba waathiriwa kwenye ajali hiyo ya moto
chanzo bbcswahili.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni