![]() |
Tume ya Mufti wa Baraza kuu la waislam Tanzania- Bakwata ya kuchunguza
na kubainisha mali,mikataba isiyofaa na rasilimali za baraza hilo ya
watu wanane iliyoundwa na Mufti hivi karibuni inaanza kazi rasmi ya
kufuatilia mali zote za bakwata zilizouzwa na kuingia mikataba ili hatua
stahiki zichukuliwe kuzirejesha mali hizo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini dsm Makamu M/kiti wa Tume hiyo
Sheikh Issa Othman Issa ametaja baadhi ya hadidu za rejea za tume hiyo
itakayofanya kazi kwa siku 90 ni pamoja na kufuatilia mikataba yote ya
Uuzwaji wa mali za bakwata ikiwemo Viwanja,nyumba za waqfu nchi
nzima,pamoja na mikataba mbali mbali ya Ubia.
Aidha Tume hiyo imewataka waislam nchini pamoja na wananchi mbali mbali
kushirikiana kwa kutoa taarifa zitakazowezesha kubaini mali zote za
bakwata nchi nzima ambazo zimeuzwa ama kubadilishwa umiliki kinyemele
ili zirejeshwe chini ya baraza kuu huku wahusika wote waliousika katika
udanganyifu huo kufikishwa ktik vyombo vya sheria.
Katika salam zake za Eid El Fitri Mwaka huu Rais Dr.John Pombe magufuri
alimtaka Mufti Sheikh Abubakar zubeir kuunda Chombo cha kubaini mali
zote za bakwata zilizouzwa au kumilikiwa na wajanja wachache ili
zirejeshwe mikononi mwa baraza hilo.
|
Tanzania Entertainment News,Politics News ,Celebrity religion and Live Updates
Jumapili, 11 Septemba 2016
Tume ya Mufti inaanza kazi rasmi ya kufuatilia mali zote za BAKWATA
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni