Kurasa

Jumapili, 18 Septemba 2016

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 7 & 8

Muandishi : Eddazaria g.Msulwa

Ilipoishia
Askari mmoja mwenye mwili mkubwa akamnyanyua Fetty na kumuweka begani mwake na safari ikaendelea.Fetty akayafumbua macho yake na kuona askari aliye mbebe ndio wa mwisho katika mstari wanao tembea,Kwa ustani wa hali ya juu Fetty akaichomeka mikono yeke katikati ya shingo ya askati,kwakutumia pigu akaanza kumnyonga askari huku akiwa amening'inia kwa nyuma.Mikoromo ya asakri ikawastua wenzake waliopo mbele kitendo cha wao kugeuka wakamkuta mwenzo ndio yupo kwenye hatua za mwisho huku macho yake akiwa ameyatoa njee

ENDELEA
Askari mmoja akataka kufyatua risasi ila mkuu wa masafara akamzuia,Fetty akaiachia shingo ya askari huku akiwa amehakikisha kwamba askari huyo yupo kwenye hali mbaya sana.Askari mmoja akampiga Fetty kwa kutumia kitako cha bunduki na kumfanya  Fetty ajikunje huku akitoa mguno mkali wa maumivu
“Kumbukeni kuwa,anahitajika akiwa hai”
Mkuu wao alizungumza
 
“Sawa mkuu,ila anahitaji kupata kibano kidogo”
Wakaendelea kumtazama mwenzo,ambaye hadi hapa alipo hali yake haipo vizuri sana.Vichwa vya askar vikaanza kupata moto kwani mwenzao ambaye alikuwa anakaribia kunyongwa ndio anaye fahamu njia ya bombo hilo japo imenyooka ila kuna sehemu mbele imegawanyika katika njia nne.Mwenzao anayejulikana kama inspector Julio hawezi kuendelea mbele na safari
 
“Mkuu kuna tatizo jengine limejitokea,Over”
“Nini tena inspector John? Over”
“Huyu binti alimkaba Inspector Julio,Over”
“Nyinyi mulikuwa wa hadi mwenzetu akabwe?”
Sauti ya mkuu wao ilizungumza huku akiwa anafoka,
“Mkuu alizimia,ndipo inspector Julio alipo amua kumbeba”
“Pumbavu zenu.Hakikisheni anatoka huyo binti,akiwa hai na Julio naye akiwa hai”
 
Fetty akatabasamu huku akiwatazama askari,kwani kwake kazi yake imeshaanza kuwa nyepesi kwani mtu ambaye anamuhofia ni huyu Inspector Julio,ambaye kwa mtazamo wake tu anaonekana ni mtu hatari sana katika swala zima la kutumia silaha.Askari mmoja akasimama mbele ya Fetty huku akiwa amempa mgongo akisaidiana na wezake katika kumpa huduma Inspector Julio,huku kazi yake ikiwa ni kuzifungua kamba za viatu vya Julio
 
Kwa umakini wa hali ya juu,Fetty akazichomoa funguo nyingi zinazo ning’inia kiunoni mwa askari huyo pasipo yeye mwenyewe kujua.Kwa bahati nzuri katika wingi wa funguo hizo zipatazo kumi na mbili,mbili ni funguo za pingu.

Macho ya Fetty yakawa na kazi ya kuwatazama askari jinsi wanavyo pata shida katika kumsaidi mwenzao ambaye hali yake inazidi kuwa mbaya.

Hakuna askari aliye kuwa na muda wa kumtazama Fetty kwani wanaamini kile kitako cha bunduki alicho pigwa kwenye tumbo,bado anaendelea kukisikilizia maumivu yake.Fetty akafanikiwa kufungua pingu za mikono pasipo askari yoyote kugundua.Akajaribisha kufungu mnyororo wa miguni ila akashindwa kwani hakuna funguo inayo ingiliana na kufuli alilo fungwa miguuni.
 
“Ja............ama..ani mmmim...i siwezi ku...pona.Ila,njia uki...oony......sha utaku...nja kulia...kwenye shimo lenye mlang....o wa....”
Inspector Julio alizungumza kwa shida na hakuweza kumalizia sentesi yake,mauti yakamchukua.

Inspector John akanyanyuka kwa hasira na kumfwata Fetty sehemu aliyo kaa.Kufumba na kufumbua akajikuta akirushwa juu kimo cha mbuzi  tena beberu na kutua chini kama mzigo.

Hii ni baada ya Fetty kuikutanisha miguu yake kwa pamoja,Kisha mikono yake aliikita chini na kujizungusha kwa kasi kubwa.Askari walio salia wakiwa wanamtizama mkuu wao.Fetty akajinyanyua kwa haraka na kumvaa askari aliye mchomolea funguo,akaichomoa bastola ya askari huyo ambaye alijitahii kumpiga ngumi  za mbavu Fetty
 
Bila ya huruma Fetty akafyatua risasi iliyo penya kwenye kichwa cha akari anayepambana naye na kumtuliza kimya.Askari watatu wa kiume wakazikoki kwa haraka bunduki zao na kuanza kuzifyatua risasi,ila kwa haraka sana kama tairi la gari liendalo kwa kasi sana,akawa na kazi ya kubiringika huku akiwafwata askari kwenye miguu yao mita chache kutoka alipo.
Akiwa anabiringika, bastola iliyopo mkononi mwake ikawa na kazi ya kufyatua risasi zilizo waangusha askari watatu chini na akabaki Inspector John na askari wa kike aliyetengenezwa kama yeye,na wakati wote tukio  la wezake kuangamizwa lilimpa kiwewe hadi akawa na kazi ya kuyaziba masikio yake akiziba asisikie milio ya risasi.Fetty akalala katikati ya miguu ya Inspector John huku mdomo bastola yake akiwa ameuweka kwenye sehemu za siri za Inspector John.Bunduki ya inspector John akawa ameilekezea kwenye kichwa cha Fetty ambaye macho yake yanatazamana na macho ya Inspector  John
“Shoot ni kushooti”
Fetty alizungumza huku akitabasama,na bastola yake akawa na kazi ya kuigusisha gusisha kwenye vitenesi vya Inspector John

 *************
Gari waliyopanda askari wapelelezi ikazidi kuongeza mwendo,huku kila mmoja akiwa na bastola yake mkononi.Kwa uelewa wao mkubwa katika kazi yao ya upelelezi wakagundua kuna gari tatu ambazo kwa Tanzania ni watu wachache sana ambao wanazimiliki kutokana na gharama zake kuwa ni kubwa sana.
“T upo tayari?”
“Ndio Y”
“l je?”
“Ndio Y”
“X je?”
“Ndio Y”
 
Askari hawa waliweza kupeana herufi za moja moja kurahisishana kuitana majina waliyo pewa kazini au na wazazi wao.

Y ndio kiongozi wao mkubwa ambaye ndio dereva wa gari hili ambalo kwa mtazamo wa bodi(umbo) lake la nje,inaonekana ni chakavu Ila injini yake na vifaa vingine ni vipya na inauwezo wa mwendo kasi 250 KM/H.

Kila mmoja akawa na kazi ya kuzitazama gari hizo zinazo wafwata kwa mwendo kama wanao kwenda nao
Rahab akiwa ametangulia gari lake mbele akawawashia wezake taa  huku akikanyaga breki za gari lake,akiwaashiria wapunguze mwendo.
 
“Baby’s munanisikia?” Rahab alizungumza kwa sauti ya kawaida
“Tunakupata”
“Wale jamaa,ninamashaka nao wamestukia dili”
“Kwa nini?” Ann aliuliza
“Kwa maana mwendo wao ni wamashaka mashaka”
“Haya sasa,Plan B yetu ni nini?” Halima aliuliza
“Kuwavamia bwana kwa pamoja” Agnes alishauri
“Tukiwavamia tutampataje Fetty?”
“Sasa ishu inakuwa vipi?” Rahab alizungumza
“Tuwafwateni tu” Anna alishauri
“Oya gari zetu,si zina map direction?”
“Ndio”
 
“Rahab wewe uliopo mbele tuambie,namba za gari la hao jamaa ni ngapi?”
“T234KSJ”
“Tuiingizeni hiyo namba kwenye hizi ramani zetu tutaweza kuiona kwa ishara hiyo gari kila inapo kwenda” Agnes alizungumza
“Sasa Ag wewe ndio mtaalamu wa hivi vitu sisi wezako wala hatujui”
“Ok,ngoja niingize”
 
Agnes akaiingiza namba ya gari na kwamsaada wa satellite aliweza kuiona gari ya wapelelezi kila inapo kwenda huku ikionekana kwa alama nyekundu.

Akawaelekeza wenzake jinsi ya kufanya na kila mmoja pembeni ya mskani wa gari lake kuna kioo kidogo kilicho unganishwa na sateliti na kazi yake ni kuweza kuonyesha ramani ya sehemu ambayo unahitaji kwenda au gari unayo taka kuifwata sehemu ilipo kikubwa ni kuweza kuzitambua namba za usajili wa gari hilo.
Wakaziendesha gari zao kwa mwendo wa kawaida na kuifanya gari ya wapelelezi kuzidi kutokomea,huku wakiwa hawana wasiwasi kuipoteza gari hiyo.

Wapelelezi wakaanza kupata matumaini baada ya gari tatu zinazo wafwata kuziacha nyuma sana.Gari ya wapelelezi ikafika Kimara Gas Station na wakashuka kwa haraka kwenye gari.Rahab na wezake wakalishuhudia gari la wapelelezi likiingia kwenye kituo cha gesi kilichopo Kimara.Wapelelezi wakaingia kwenye msitu wa miti ulipo hapo ambapo ndipo lilipo shimo ambalo wanatarajia kuwapokea Fetty na askari wengine
“Jamani tusishuke kwanza” Agnes alizungumza
“Kwa nini?”
 
“Hamuwezi kujua kama jamaa wamejificha wanatusubiria tushuke watushambulie”
“Hapo,umezungumza point”
Wakazisimamisha gari zao mbali kidogo na kilipo kituo cha gesi,wakisubiria kufanya kazi moja tu ya kuwashambulia askari hao pale watakapo mchukua Fetty
***************
Inspector Julio akaanza kutetemeka huku akimeza mafumba ya mate,kwani ni mwaka wa 25 sasa analitumikia jeshi la polisi,ila hajawahi kukutana na mwanake hatari kama Fetty.Kwa woga akajikuta akiminya kitufe cha kuziruhusu risasi kutoka,kwa bahari mbaya bunduki yake tayari imeisha risasi.
“Kwaheri”
 
Fetty alizungumza huku akiziruhusu risasi mbili kuchomoka kwenye bastola yake aina ya ‘browningu SFS’ na kuzichangua sehemu za siri za Inspector John,Fetty akasimama na kumtazama askari wa kike anaye fanana naye kuanzia mavazi hadi sura ya bandia aliyo valishwa.Fetty akataka kumuua  askari huyo ila akasitisha zoezi lake na kumnyanyua
“Nipe funguo nijifungue”
“Zip.....o kwa inspector John”
 
Fetty akamtazama kwa umakini askari,akachuchumaa kwa umakini huku bastola yake akiielekeza kwa askari huyo anaye itwa Rehema.Akaipapasa mifuko ya Inspector John na kuzitoa fungua nyingi.Akachagua funguo moja inayoweza kufungua kwenye mnyororo,kwa bahati nzuri akaipata.Akajifungua na kumuomba Afande Reheme kutangulia mbele huku akiwa ameshika tochi inayowasaidia kuona mbele.Wakafika kwenye njia nne tofauti,wakabaki wakiwa wamesimama wakiwa hawajui ni wapi waende
“Sema njia  ni ipi?”
“Sujui hata mimi”
 
Fetty akampiga kofi la shavu Afande Rehema huku akiwa amemnyooshea bastola
“Sema ni njia gani la sivyo nakumwaga ubongo?”
“Hii.....”
 
Afande Rehema alizungumza ili mradi aepukane na kifo cha kupigwa risasi.Japo amejitamkia ila njia aliyo ionyesha ndio sahihi.Wakaendelea na mwendo wao hadi wakafika sehemu yenye ngazi za chuma za kutokea nje.Fetty akamtanguliza afande Rehema japo amefungwa pingu za mikononi ila akajitahidi hivyo hivyo kuanza kupanda kwenda juu
 
*****************
Milio ya risasi waliyo isikia kupitia redio ya upepo,iliwachanganya sana wakuu wa polisi na kuwafanya waanze kubabaika na kuwapa taarifa wapelelezi kuwa kuna hali tete ambayo inaendelea chini walipo askari.

Mbaya zaidi kila wanapo jaribu kuwasiliana na wenzao hawakuweza kupata jibu la aina yoyote.Wapelelezi wakajiandaa kwa chochote kitakacho jitokeza kwenye shimo huku bastola zao wakiwa wameziandaa kwa umakini wa hali ya juu
Wakauona mfuniko wa shimo,ukifunguliwa na kichwa cha Afande Rehema kikatokeza,
“Musiniue”
 
Afande Rehema alizungumza huku akijitoa kwa kasi kwenye shimo.Fetty akajua kuna hali ya hatari ipo juu,akaishika bastola yake vizuri na kupandisha ngazi kwa hataka kabla hajajitokeza juu akakiona kichwa cha mpelelezi mmoja akichungulia,Mpelelezi akiwa anashangaa kati ya Rehema na Fetty yupi ni muhalifu kwani wanafanana,akastukia risasi ikipiga kwenye paji la uso wake na kumuangusha chini
 
Milio wa risasi ukawastua Rahab na wenzake,kwa haraka wakawasha magari yao na kuyasimamisha pembeni ya kituo cha gesi.Wakashuka kwa haraka kila mmoja banduki yake ikiwa mkononi.
Walinzi wa kitua cha gesi wakazidi kuchanganyikiwa kwani mlio huo wa risasi umesikika nyuma ya kituo na watu walio ingia kwenye  kituo chao hawaeleweki.Mlinzi mmoja akaikoki bunduki yake aina ya gobora,kitendo cha mlinzi kuishika bunduki yake,Anna alikiona vizuri,pasipo kuuliza ni nini mlinzi anataka kukifanya,akafyatua risasi iliyo muangusha mlinzi chini.Walinzi wengine wakalala chini kwa woga baada ya kumouona mwenzao akivuja damu nyingi
 
Wapelelezi wakabaki katika hali tata,huku kila mmoja akikataa kwenda kuchungulia kwenye shimo asije akakutwa na ktu kilicho mkuta X.

Wakiwa katika taharuki risasi zisizo na idadi zikatua mwilini mwao zikitokea nyuma yao na ukawa ndio mwisho wa maisha yao.Agnes akanza kupiga hatua za haraka akimfwata Afande Rehema aliye lala chini
“Fetty nyanyuka tuondole”
 
Fetty alianza kushua ngazi kurudi kwenye shimo ila baada ya kuisikia milio mingi ya bunduki.
“Fetty twende”
Agnes alizidi kumuita Afande Rehema baada ya kumuona anababaika.Kabla Fetty hajamalizi kushuka kwenye ngazi ya mwisho kuingia kwenye shimo akaisikia sauti ya Agnes.
“Agnes huyo sio Fetty ni polisi mimi nipo humu”
 
Fetty alizungumza huku akianza kupanda ngazi kwa haraka,Agnes akabaki akiwa ameshangaa,akamuona Fetty akichomoza kichwa kwenye shimo.Afande Rehema akajaribu kuiokota bastola ya askari mmoja aliye anguka chini.Risasi kama sita zikatua mgongoni mwake kutoka kwa Rahab.Fetty akamkimbilia Agnes na kumkumbatia
“Pole shosti”
“Asante”
 
Kabla hawajaondoka,mwanga mkali wa helcopar ya polisi iliotumwa kufika kwenye eneo hilo,ukaanza kuwamulika.Wakaanza kukimbia wakielekea mbele ya kituo walipo ziacha gari zao, kitendo cha Halima kujitokeza wakakutana na gari zipatazo kumi za polizi zikiwa zimetanda mbele ya kituo na askari wengi wakiwa na bunduki zao wakiwa wameelekezewa wao.
“WEKENI SILAHA ZENU CHINI”
“Shitii”
 
Wote watano wakabaki wakiwatazama askari huku helcopar ya polisi ikiwa inawamulika kwa mwanga mkali mweupe ambao umelifanya eneo walilo simama wao kuwa kama mchana na endepo watafanya kitu chochote cha kijinga,askari wenye bunduki wapatao thelasini wenye bunduki watazifyatua risasi zao pasipo kuwa na huruma
Endelea na sehemu ya 8 kupitia ubuyublog.com 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni