Kurasa

Jumapili, 18 Septemba 2016

Mkuu wa Mkoa wa Dsm Paul makonda amezindua Muonekano mpya wa waendesha Bodaboda na bajaji katika Mkoa wa DSM

Mkuu wa Mkoa wa Dsm Paul makonda amezindua Muonekano mpya wa waendesha Bodaboda na bajaji katika Mkoa wa dsm ambapo hivi sasa watakuwa na Mavazi maalum ya kuwatambua,Vituo sambamba na namba maalum katika mavazi yao ili kuboresha huduma hiyo na kuwatambua wahalifu wanatumia bodaboda kutekeleza uhalifu wao.
Aidha Makonda amezindua chama cha madereva na wamiliki wa pikipiki na bajaji katika mkoa wa dsm chenye wanachama 45,000/= ambapo amewataka kuheshimu sheria huku serikali,jeshi la Polisi pamoja na Sumatra ikiweka mpango madhubuti wa kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa.
Akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika katika viwanja vya leaders kinondoni,Makonda amesema kuanzishwa mfumo huo mpya ambapo kila wilaya madereva hao watambulika kwa mavazi yao,namba kutasaidia kupunguza changamoto za uhalifu,lakini kuwezeshwa kupitia chama chao.
Katibu wa Chama hicho Daudi Ali amesema wamepokea Mpango huo na kuahidi kushirikiana na Serikali ya Mkoa na jeshi la Polisi mkoa wa dsm kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa kuzingati
Chanzo:muungwana blog

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni