Kurasa

Jumapili, 25 Septemba 2016

Kugundulika kwa matumizi ya nishati ya gesi asilia serikali imekoa zaidi ya shillingi trillion 14

Kutokana kugundulika kwa matumizi ya nishati ya gesi asilia nchini  mpaka sasa serikali imekoa zaidi ya shillingi  trillion 14 mwaka 2014-2015 ikiwemo kuwepo kwa umeme wa uhakika hapa nchini.

Akitoa mada wakati wa swmina kwa waandishi wa habari mkoani Morogoro juu ya mafanikio ya kupatikana kwa gas tanzania  mhandisi wa shirika la maendeleo ya petrol  Tanzania TPDC Felix 


 Nanguka amesema shughulli nyingi za kiuchumi zimehamia katika matumizi ya gesi  na kupunguza  gharama kubwa za  matumizi ya mafuta mazito  hali iliyopelekea kuzalishwa kwa umeme wa gesi kuenea katika viwanda vikubwa na vidogo huku akidai tafiti zanaonyesha kuongezeka kwa pato la taifa baada ya kukamilika kwa mitambo yote ya gasi.

Aidha  afisa uhusiano wa shirika la maendeleo ya petrol tanzani TPDC  Francis Lupokela amesema  katika shughuli za ujenzi na ulinzi wa miundombinu ya kusafirishia gesi asilia hapa nchini shirika la limewanufaisha wananchi katika upatikanaji wa ajira nae mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari morogoro Nicksoni Mkilanya amesema mafunzo hayo yatawasaisdia waandishi kuhamasisha na kuandika habari za mafuta na gesi kwa ueledi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni